Back
William Ruto
President, Kenya

RUTO IS BACK! Listen to his Speech today in Statehouse Destroying Gachagua, Matiangi, Kalonzo Sifuna

🎥 Jun 12, 2026 📺 Kenya News Channel ⏱ 67m 👁 3590 views
Kenya News Today from Nairobi and Africa. Get more at Citizen TV Live Streaming Kenya Now, NTV Kenya Livestream and KTN News Live. For more Latest News Alerts and Updates subscribe to our YouTube Channel:    / @kenyanewschannel   Follow us on Social Media: Website: https://kenyanewschannel.co.ke Facebook:   / kenyanewschannel   Instagram:   / kenyanewschannel   X Twitter: https://x.com/KeNewsChannel TikTok:   / kenyanewschannel   Contact us on Email: [email protected] Check out: Citizen TV Kenya:    / @kenyacitizentv   #KenyaNewsChannel #KenyaNews #CitizenTV...
Watch on YouTube

About William Ruto

President William Ruto has been engaged in a series of domestic and international engagements. In Kenya, he hosted leaders from Marsabit County at State House, where he discussed development projects including the construction of a new airport and road infrastructure, and emphasized his administration's focus on education and healthcare funding. He also received the Gor Mahia football club after they won the Premier League, congratulating them and announcing plans to complete 28 new stadiums across the country. At a National Prayer Breakfast, Ruto stated that he would accept the outcome of the 2027 election and dismissed claims of a plot to rig the polls, saying the elections would be "free and fair" and conducted without violence. He also assented to three bills, including the National Disaster Risk Management Bill. Internationally, Ruto traveled to South Africa for bilateral talks with President Cyril Ramaphosa, where they discussed trade, migration, and cooperation in pharmaceutical manufacturing. He also addressed Kenyans in Finland, stating that he had engaged with European partners on an economic partnership agreement and that Kenya was in the process of establishing a sovereign wealth fund. In various public addresses, Ruto has highlighted what he described as economic improvements under his administration, including a reduction in inflation, a stronger foreign exchange reserve, and increased funding for education and healthcare. He has also criticized the opposition, stating that they "have no new ideas" and lack a development agenda.

Source: AI-verified profile updated from William Ruto's recent appearances. Browse all interviews →

Transcript (35 segments)
✨ AI-enhanced transcript with speaker attribution
W
William Ruto0:00
Your excellency. Haya asante sana Abshiro, tafadhali tunaweza keti. Ndugu wananchi wa Marsabit, hamjambo?
A
Audience0:13
Hamjambo.
W
William Ruto0:14
Marshabet hoye.
A
Audience0:16
Hoye.
W
William Ruto0:17
Bultinagaada. Ah, mimi nimefurahi sana. Najua, mimi nimefurahi sana. Mimi wacha nichukue nafasi hii kwa mara ya kwanza niwakaribishe watu wa kutoka kaunti ya Marsabit hapa katika State House. Karibuni sana. Nasema karibuni tena. Najua ya kwamba watu wengi wamenitembelea hapa State House kutoka counties nyingi, lakini nilisema liwe liwalo, lazima pia watu wa Marsabit wafike hapa State House. Jameni, mimi naelewa ya kwamba kutoka Moyale kufika hapa ni mbali sana. Naelewa, lakini na najua pengine kulikuwa na matatizo, sijui tutafika namna gani, sijui itakuwa namna gani, lakini nimefurahi sana kuwaona. Karibuni. Hii State House ni yenu kama vile ni ya Wakenya wale wengine wote. Na furaha yangu ni kwamba leo watu wa kutoka kaunti ya Marsabit, watu wa kutoka mbali kule Sololo, watu wa kutoka kule Maikona, sijui Dukana, Loyangalani, sijui watu wa Ileret wako hapa kweli?
A
Audience2:19
Eh, mi naona watu wa Ileret wako area.
W
William Ruto2:21
Karibuni sana. Mimi nilikuwa ni mwisho ya dunia huko mahali ingine, so mimi nimefurahi sana mmefika, na karibuni. Najua wengi wangependa kukuja lakini of course usafiri, masaa, magari imewazuia wale wengi, lakini wale waliofika hapa mmefika kwa niaba ya wale wengi ambao wako nyumbani. Na mimi nitachukua nafasi yangu nikuje niishi huko Marsabit. Unajua, Marsabit sio mahali pa kuja siku moja na kurudi, unakuja unakaa huko, na niko na hiyo mpango. Kwanza, mimi mbali na kusema karibuni hapa, nataka niwashukuru sana kwa urafiki wenu, ushirika wenu, na kwa kura mliyonipatia nikawa Rais wa Kenya. Mimi narudia tena na tena nikisema asanteni sana kwa kura zenu. Na niwahakikishie ya kwamba mimi nitafanya bidii ili kura mliyonipatia iweze kuwa faida kwenu na faida kwa wananchi wa taifa letu la Kenya. Na sababu hiyo ndio nimebadilisha mambo mengi. Nataka tu niwaambie mambo matatu ama manne, alafu niseme mambo ya Marsabit, alafu niwaeleze vile tutasonga mbele pamoja. Ya kwanza, mlinipatia nafasi wakati tulikuwa na matatizo makubwa sana ya uchumi. Tulikuwa na madeni kibao. Tukawa na matatizo ya inflation, tukawa na matatizo mengine mengi. Lakini mimi nilikuja hapa nikaketi chini na wale ambao niliwapatia nafasi ya kushirikiana na mimi katika uongozi wa Kenya. Tukarekebisha mahali kulikuwa na matatizo. Tukapunguza madeni ambayo yalikuwa yanakopwa kila wakati. Tukashukisha maneno ya inflation nchini. Leo nikisimama mbele yenu hapa, uchumi ya Kenya iko mahali pazuri kuliko vile ilivyokuwa 2022. Kwa wale ambao nyinyi ni wasomi, and I say this without fear of any contradiction. Kwa wale ambao nyinyi ni wasomi, 2022 Kenya ilikuwa imeorodheshwa kati ya nchi ambayo itashindwa kulipa madeni yake, among six countries that were expected to default on their foreign financial obligation. Lakini mimi nilisema nikiwa Rais wa Kenya, it will not happen. Na Mungu ametujalia. Kwa nchi sita ambazo zilikuwa zimeorodheshwa ya kwamba itashindwa kulipa madeni, ni Kenya yake out of the six. Five countries defaulted. It's only Kenya that is not default. And today, uchumi yetu leo tumefanya bidii. It is the sixth largest economy in Africa. We have reduced inflation. We have reduced exchange rates. Dola ilikuwa 160 something, sasa dola ni 129. We have made sure our economy is stable. Pesa ambayo tuko nazo za kigeni, ile inaitwa Foreign Exchange Reserves, ilikuwa bilioni 5.7, leo ni bilioni 13 ambayo tuko nayo. So uchumi ya Kenya is more stable than we were in 2022, and that is the correct position. Na ni kwa sababu niliwaeleza tutapanga mambo ya uchumi, kwa sababu tusipopanga mambo ya uchumi, Kenya itaenda mahali ambapo si pazuri. Jambo la pili, niliwaeleza vile vile ya kwamba nitapangana na mambo ya kilimo. Nyinyi mnajua, wakati nimechaguliwa watu walikuwa hapa kwa street wanatembea na sufuria kwa kichwa wakisema bei ya unga. Nyinyi mli pengine hamkusikia kwa sababu mko mbali, hapa street kulikuwa na balaa kubwa. Unga ilikuwa 250 per 2 kg, nini matatizo. Na mimi nikawaeleza ya kwamba njia ya kuhakikisha kwamba kuna chakula katika taifa letu la Kenya ni kubadilisha ama kutransform mambo ya kilimo, sio kusubsidize ile inaitwa consumption, lakini ni kusubsidize production. Bei ya mbolea tukapunguza. Wakora wale walikuwa wanatusumbua na mambo ya utapeli, brokers ambao walikuwa wamekuwa ndio wenyewe kule kwa makampuni ya sukari, kule kwa kahawa, kule kwa chai, tukawaondoa. Tukahakikisha kwamba kila mkulima tumemsajili. Leo, leo katika taifa letu la Kenya tumeongeza mapato yetu ya chakula. Mahindi tumeongeza kutoka magunia ya milioni 40, sasa tumefikisha milioni 70. Kahawa iliyokuwa inauzwa shilingi 50 kwa kilo, leo inauzwa 120. Ile makampuni ya chai, ile makampuni ya sukari ambayo ilikuwa imekwama, tumezikwamua. Kampuni hizo sasa zinaendelea, na kufikia miaka miwili mitatu, badala ya Kenya kuagiza sukari kutoka nje, tutakuwa tunauza sukari kutoka Kenya. So we have transformed our agricultural sector. Today we can confidently say as a nation we are well on course towards being a food secure nation. We are increasing our exports of tea. We are increasing our exports of coffee. Um, mimi nimetoka leo asubuhi Europe kupanga na wale ambao wananunua chakula yetu ama vifaa yetu. Wale wananunua kahawa, wale wananunua chai, wale wananunua maua na horticulture. Na tumekubaliana na wao vile tunasonga mbele. Mnajua, watu wa Finland, mahali nimetoka leo asubuhi, ndio wananunua ama ndio wanakunywa kahawa number one in the whole world. Belgia, mahali nilikuwa juzi, ndio nchi ambayo inanunua kahawa ya Kenya. The highest today is Belgium, and it is good for us to engage with them so that we can secure our markets. So tunaendelea namna hiyo, na hiyo ndio kazi yangu kuhakikisha ya kwamba Kenya inaheshimika na Kenya inafanya biashara kila sehemu ya dunia hii yetu. Ya tatu, tulikubaliana mambo ya elimu. Nyinyi mnajua ya kwamba elimu ndio jambo la muhimu kuliko mambo yote. Ndio inatuletea usawa, watoto wa maskini na watoto wa tajiri wanakuwa sawa wakipata elimu. Tulikuwa na matatizo matatu 2022 kwa mambo ya elimu. Tulikuwa na upungufu ya walimu zaidi ya 116,000. Tulikuwa na madarasa chache. Funding model ya watoto wetu ilikuwa chini, na tulikuwa na shida ya CBC. Mimi nimefika hapa ofisini kwa kura zenu na kwa maombi yenu. Na haya mambo manne ambayo yalikuwa yanatusumbua tumeyatatua. Number one. Tumeajiri walimu 100,000 in the last 3 years. Sikizeni watu wa Marsabit. Hakuna serikali imeajiri walimu 100,000 in 3 years tangu independence. In other words, kwa wale walimu tuko nao 400,000 Kenya, a quota 100,000 tumewaajiri in the last three years. Why? Sababu gani tumefanya hivyo? Kwa sababu elimu ni ya muhimu. Ndio inatuletea usawa. Kila mtoto wa Kenya aende shuleni, lazima apatane na mwalimu. Tumejenga madarasa 23,000 kuhakikisha kwamba there are enough learning spaces. Tumehakikisha ya kwamba ile funding model ya watoto wetu inajali kila mtoto wa Kenya. Hata wale watoto kutoka jamii maskini wanapata nafasi sawa wakienda university, wakienda TVET, kwa sababu tumeongeza pesa ya kusomesha watoto wetu. Budget jana ilisomwa. Jana bajeti ilisomwa. Pesa ambayo tumeongeza ya watoto wetu kusoma in 2022 ilikuwa bilioni 500. Bajeti iliyosomwa jana ni bilioni 767 ambayo tumeongeza kuhakikisha kwamba watoto wetu wanasoma. Saa zingine unasikia watu wengine wanasema oh there is a crisis in education. You know you wonder, how is there crisis in education today when we have hired 100,000 teachers, when we have increased the budget of education from 500 million to 767 million, when we have built an additional 23,000 classrooms, when we have straightened the CBC into now a competence-based education and training, and when we have enhanced our budget for our university education especially help from 18 billion shillings to 56 billion shillings. You know, people must be honest and must be truthful. Hiyo kiwanja ya elimu tumeinyorosha vizuri, kwa sababu mimi naamini ya kwamba hatutaki hata mtoto mmoja Kenya akose nafasi ya kusoma. Na mimi nawauliza nyinyi watu wa Marsabit kwa heshima kubwa. Nyinyi kama wafugaji, tafadhali tunaweka pesa nyingi sana kusomesha watoto wetu. Usikubali wewe kama mzazi. Watoto wengine wanaenda shuleni, mtoto wako umeenda umemwambia aende achunge mbuzi, aende achunge ng'ombe, aende achunge ngamia. Hiyo unajirudisha nyuma na unarudisha nyuma taifa letu la Kenya. Kila mtoto awe shuleni, na tumeamrisha chiefs, assistant chiefs, wazee wa mitaa, na kuanzia mwezi huu wa saba, hata wale wazee wa nyumba 10 sasa tutakuwa tunawapatia marupurupu kidogo ndio waweze kusukuma maneno ya serikali na kuhakikisha ya kwamba watoto wetu wote wako shuleni. Mimi vile vile niliwaahidi ya kwamba tutabadilisha mfumo wetu wa matibabu. Pale nyuma, matibabu ilikuwa imeanza kuwa starehe ya watu wenye wako na kazi, wale wako na ajira, wale wako na uwezo. Ili hali kila mtu anakuwa mgonjwa. Ndio nikasema tunabadilisha mfumo wa mambo ya matibabu. Tunataka kila Mkenya apate nafasi ya kutibiwa. Pale nyuma kulikuwa na mipango ya NHIF. NHIF ilikuwa ni lazima uwe na kazi, lazima uwe na pesa, lazima uwe uko na uwezo wa kulipa. Leo nimesema kila Mkenya asajiliwe ndani ya SHA, na pesa. Awe na kazi asiwe na kazi, awe na uwezo asiwe na uwezo. Kila mwananchi wa taifa letu la Kenya. Katiba ya Kenya inalazimisha serikali kuhakikisha ya kwamba kila Mkenya anapata nafasi ya kutibiwa. Sio lazima uwe na kazi. Sio lazima uwe na uwezo, sio lazima uwe na pesa. Ni haki yako kama Mkenya kupata matibabu. Na mimi nimefurahi tumeungana na counties, tumeungana na wale wengine wote other stakeholders. Leo, wale watu waliokuwa wamesajiliwa ndani ya NHIF watu milioni nane, leo tumefikisha watu milioni 31 waliosajiliwa katika bima ya afya. Na nia yetu ni kuhakikisha ya kwamba hakuna Mkenya tena atauza shamba yake, ng'ombe yake, ngamia yake, mbuzi yake ati kwenda kulipa gharama ya hospitali. Tunataka gharama ya hospitali ilipwe na bima ya afya inayosimamiwa na serikali. Nyinyi mnanielewa jameni? Na ndio mimi nataka niwaulize, kila mmoja wetu najua bado kuna mahospitali zingine huko kando kando bado wanauliza pesa wananchi, na ndio tumesema wewe kama mwananchi ujue, na nimesema hapa sio leo sio mara moja, ya kwamba afya ni haki ya kila Mkenya, na hakuna Mkenya atanyimwa nafasi ya kutibiwa ama dawa kwa sababu hana pesa, kwa sababu hiyo gharama inalipwa na serikali ya Kenya. So mimi nataka nimuulize gavana wetu na viongozi wengine wote, bado watu wengi wa Marsabit hawajajiandikisha kwa SHA. Bwana, ukienda kaunti kama ya Mombasa, 85% ya watu wa Mombasa wamejiandikisha kwa SHA. Bado mko karibu 30%. Kwanza nyinyi ambao mnanisikiza hapa mmejiandikisha kwa SHA kweli? Eh.
Hebu nione wale wamejiandikisha kwa SHA wainue mkono. Eh, unaona bado iko maneno hapa kidogo? Eh, nyinyi tafadhali kila mmoja wenu mjiandikishe kwa SHA. Ukijiandikisha kwa SHA tutafanya, tutapata nafasi ya kufanya mambo matatu: ya kwanza, tutapanga madawa ya kutosha; ya pili, tutapanga madaktari wa kutosha; na ya tatu, tutapanga vifaa ambayo itatumika hospitalini kuwatibu ya kutosha. Usipojiandikisha, unafanya kazi yetu ya kupanga madawa, madaktari pamoja na vifaa vya kutibu wananchi kuwa ngumu. We need data. Tunahitaji data ya kuhakikisha kwamba kila mwananchi tuko na wananchi kiasi fulani, hospitali fulani tuko na wananchi kiasi fulani, sehemu fulani ndio tuweze kupanga mambo ya madawa, mambo ya matibabu. Jameni, mtanisaidia kuhamasisha wale wananchi wote wengine wajiandikishe kwa SHA. Nawaomba, kwa sababu ni faida kwenu. Mkishajisajili, ndio tuweze kutembea hiyo barabara tukiwa pamoja. Mimi vile vile, ningependa kusema ya kwamba sisi tunaelewa ya kwamba tuko na nafasi chache za ajira, na tulikubaliana na nyinyi ya kwamba tutakuwa na mpango wa vile tutapata nafasi na kupanua nafasi ya ajira kwa vijana wetu wa Kenya. Zaidi ya vijana milioni moja wanatoka shuleni kila mwaka, na hatujakuwa na mpango kamili wa vile hawa vijana wetu watapata kazi, kwa sababu kupatikana kwa kazi lazima kuwe na mpango, lazima kuwe na taratibu, lazima kuwe na sehemu hawa vijana watapata kazi. Na ndio tulikubaliana tufanye mambo manne ya muhimu ndio nafasi ya vijana wapate kazi. Number one, tuwe na program kubwa ya public infrastructure inayohusika na mambo ya housing, kujenga masoko, kujenga hostels, barabara, public infrastructure. Na hiyo kazi inaendelea. Na kupitia kwa hiyo mpango ya affordable housing, mkienda wale ambao mna relatives Nairobi na counties na town zingine zetu zote, saa hizi tunajenga nyumba 300,000 Kenya. Tumeajiri vijana zaidi ya 700,000 katika hiyo mpango. Masoko ndio hiyo tunajenga. Hostels ya vijana wetu ndio hizo tunajenga ili tuhakikishe kwamba nafasi ya ajira inapatikana. Mimi nimekuwa Belgium kuongea na watu wa EU, kwa sababu tuko na nafasi kubwa ya mambo ya business process outsourcing, ama kazi ambayo inapatikana katika mitandao. Tayari vijana 3,000 wanafanya kazi hiyo. We want, tunataka kuongeza vijana wanaofanya kazi pale wafike milioni moja. Na ndio sababu hiyo nilienda kuongea na watu wa EU, kwa sababu kuna kitu inaitwa data adequacy ambayo tumekuwa tukiongea na wao ndio tuwe na mpango ya kutosha. Kenya na European Union tumekubaliana na wao kufikia mwezi wa tisa hiyo kazi itasonga mbele, kufikia Januari next year tutakuwa tumeikamilisha, ndio tupanue nafasi ya vijana wetu ambao wanafanya kazi katika mitandao, digital jobs, digital commerce, business process outsourcing, ndio tuhakikishe kwamba teknolojia na kazi ambayo ya future, unajua ajira za siku zijazo itakuwa inategemea teknolojia, itakuwa inategemea sehemu ya digital, na Kenya haiwezi kubaki nyuma. So um, we have now concretized agreement between Kenya and the European Union. When I was there in Brussels, we have agreed on data adequacy that this will go to the European Parliament in the course of this the next two three months, and hopefully we can clear it by early next year so that we can expand the opportunities in our digital commerce, in data centers, deploying technology, so that we can create more opportunities for the young people of Kenya to work, including those from Marsabit. Nyinyi mnanielewa jameni? So hiyo kazi yote tunaendesha, na ni haki yenu kujua kama mtu ambaye mlinipatia nafasi hii ya kuwa kiongozi wa taifa letu, ni vizuri niwaeleze ni kazi gani inaendelea, si ndio? So hiyo ndio kazi ambayo tulishirikiana na nyinyi na nikawaeleza tutabadilisha taifa letu la Kenya. Mimi nataka niwahakikishie, taifa letu la Kenya litabadilika. I am very confident, hii Kenya itakuwa nchi ya maana sana. Na mkisikia ya kwamba tutakuwa first world in the next generation, msikuwe na wasiwasi, tutakuwa first world. Yes. Sikizeni. Nilikuwa nilienda juzi nilikuwa Norway, na nikapata nafasi ya kuongea na Prime Minister wa Norway. Nikapata nafasi ya kuongea na Waziri wa Fedha wa Norway. Norway ni nchi ambayo iko na sovereign fund ya trillion. Na hiyo sovereign wealth wamejenga. Saa hizi katika Kenya tunamalizia kujenga Sovereign Wealth Fund ya Kenya. Pengine nitaweka sahihi in the next one month or two months, ndio sasa hata sisi tuanze kujipanga vile wengine walijipanga kutafuta utajiri ambayo itatusaidia kuendesha miradi yetu ya maendeleo na kuondoa umaskini katika taifa letu la Kenya. Mnanielewa? Kwa sababu najua, uongozi ni kitu ya muhimu. Wale walijipanga leo. Nchi ya South Korea, nchi ya Singapore, nchi hiyo ya Norway, nchi ile ingine ya Malaysia walikuwa pamoja na sisi miaka 60 iliyopita. Leo wako first world, bado sisi tunang'ang'ana huku chini. Tofauti ni uongozi. So tukijipanga vizuri na tuamue mambo vizuri, hii Kenya tutaibadilisha. Na ni nia yangu kuhakikisha kwamba tunabadilisha hii Kenya. Unajua, watu wengi hawakuamini. Ndio mlikuwa mnasikia wanasema oh huyu William Ruto anatuambia uongo, sijui anatuambia uongo. Walisema haiwezekani kuajiri walimu vile nilisema tutaajiri. Leo tumeajiri walimu 100,000. We have transformed our education the same way I had committed. Niliwaeleza ya kwamba tutabadilisha kilimo, hawakuamini wakasema eti ni uongo. Leo kilimo imebadilika. Walisema ya kwamba mambo ya SHA, mambo ya universal health coverage haiwezekani, ati ni uongo. Leo kwa macho yetu watu milioni 31 wako ndani ya SHA, inabadilika. Ni kweli ama si kweli? Yes. So mimi nataka niwahakikishie wale watu wote ambao walikuwa wanaamini ya kwamba haiwezekani, we are going to prove to them that it is possible to change our nation. Tunaelewana jameni? Yes. Hawakuamini ati tunaweza kubadilisha kilimo. Leo kilimo imebadilika. We have done what no other administration has done. We've hired enough teachers. We've changed the funding model. We built more classrooms. We've straightened CBC. We are moving forward as a country. So I just want to assure this great nation of ours, including the great people from Marsabit, that we are going to change our nation. Wale ambao walikuwa wananiita majina, kuna siku watakuja kusalimu amri, si ndio? Yes. Wengine waliita Zakayo, sijui Zakayo. Sasa hiyo Zakayo waliniita, si watu vijana 640,000 wanafanya kazi kwa affordable housing? Si tunajenga soko 500 Kenya? Si tunajenga hostels ya vijana wetu 180? Tuendelee ama tuendelee?
A
Audience32:08
Tuendelee.
W
William Ruto32:09
Mnasema tuendelee ama tuendelee?
A
Audience32:11
Tuendelee.
W
William Ruto32:12
Si walikuwa wanasema haiwezekani. Mambo ya kilimo niliwaeleza ya kwamba tutabadilisha kilimo, wakasema ati ni uongo. Leo mbolea ilikuwa 7,000, sasa ni 2,500. Mahindi tulikuwa tunazalisha milioni 40, sasa tunazalisha milioni 70. Bei ya kahawa ilikuwa shilingi 50, sasa ni 120. Tuendelee ama tuendelee? Si tunaelewana? That's what we are doing. Na hivyo ndivyo Kenya inabadilika. Niliwaeleza ya kwamba tutabadilisha hii dunia yetu. Unajua tumekuwa tukiongea kwa mfano, hapa Bomas of Kenya tulikuwa tunaongea tutajenga. Hii KICC ilijengwa 1972. Tumekuwa tukizungumzia kujenga Bomas of Kenya for the last 30 years. Mimi nawahakikisha Bomas of Kenya mpya iko tayari, na itasonga, itasonga, itasonga hii Kenya. Airport yetu hapa ilijengwa sijui 1972. Tulijaribu kujenga ingine, wakaleta kelele, nini nini nini mpaka saa hizi airport yetu iko canvas kwa JKIA. Tuko na aibu nyingi. Lakini nataka niwahakikishie, mwezi huu wa saba tunaanza kujenga airport mpya, na tuko na vile na pesa ya kujenga hiyo airport. Kwa sababu tunataka kubadilisha Kenya. Bwana, Kenya lazima inabadilishwa na miradi na mipango ya maendeleo. Haibadilishwi na matusi. Haibadilishwi na kuitana majina. Haibadilishwi na hiyo na ingine yote. Na sikizeni, hawa ambao wanajifanya ati wanataka kushindana na sisi ni watu wako chini sana. Wako chini, wako down. Sikizeni, niwaeleze. Watu wa Marsabit, tunaelewana? Yes. Lakini wacha niseme kuna mambo. Gavana wenu na nimeongea na hawa viongozi wote, nimeongea na hawa viongozi wote na tumekuwa tukiongea mambo ya Marsabit, vile tunapanga mambo ya Marsabit. Kuna maneno kama manne hivi ya muhimu mmeniuliza. Jambo la kwanza ni barabara zenu. Pale barabara zenu. Mnajua kuna barabara tuliyoanzisha hapo before the last election, barabara ya Marsabit kwenda Segel. Hiyo ya Segel ilikuwa imekwama. Mimi nimelipa shilingi 1.4 billion kukwamua hiyo barabara na kuhakikisha kwamba inakamilishwa. Tuko na barabara vile vile iliyoanzishwa ya Second My Corona mpaka ifike na sparrows ya town, pia ilikuwa imekwama. Nimetoa shilingi 1.8 billion kukwamua hiyo barabara na kuhakikisha kwamba tutaikamilisha. Na barabara za town hapo Maikona, hiyo tutaitengeneza. Tuko na barabara ambayo ilianzishwa ikakwama pia, ya kutoka A kwenda Bute mpaka Tanaba. Tanaba, si ndio? Contractor amehangaika hapo. Na kwanza huyo contractor alikuwa msumbufu sana. Sasa nimesema huyo contractor wacha nitafutie kazi ingine, wacha nilete contractors wengine. So tumegawa hiyo barabara ndio itembee haraka. Tumesema badala ya kuwa one contract, wacha tubadilishwe iwe three contracts, ndio tuwe na contractors watatu, ndio barabara hiyo itembee haraka. Si namna hiyo? So tumesema tutatafuta contractor moja kutoka A kwenda mpaka Bute. Na sikizeni, hii eh, Jumanne inayokuja, Tuesday, ndio tunataka tunatangaza kandarasi. Tayari nimeweka pesa ya kwanza shilingi milioni 300 kutengeneza hiyo barabara. Kutoka tena Bute kwenda mahali inaitwa Garar, hapo tukiwa Gurar kuelekea kule Wajir North pia, tunatangaza kandarasi ingine ndio iweze kutembea Tuesday. Na kutoka Gurar kwenda mpaka Danaba pia tunaweka kandarasi mwingine mpya, a different one. Hiyo barabara yote tuweze kukamilisha, kwa sababu tukiweka contractor moja atachukua muda mrefu. So tukasema tugawe mara tatu ndio hiyo barabara iweze kutembea haraka. Na tumekubaliana na hawa viongozi. Mmeniambia pia kuhusu ile barabara tulitengeneza kutoka Kaisut kwenda Ngurunit. Tulitengeneza hiyo barabara lakini tulitengeneza low volume, sasa imeraruka raruka kidogo. So nitarekebisha hiyo barabara, nitaweka overlay. Nimeambia waziri wetu afanye hivyo. Alafu sasa kutoka Ngurunit kwenda wapi? Loyangalani. Si ndio? Lakini hii ya Loyangalani iko mbali bana. Eh, mtanikubalia nifanye step mbili, si ndio? Nitangaze anata 50 km kwanza, alafu niongeze hiyo ingine ifike Loyangalani. So pia, on Tuesday tunatangaza hiyo kutoka Ngurunit tuanze sasa kusukuma iende, iende Loyangalani, tutamalizia hapo katikati. Na kuna security roads zingine ndogo ndogo ambazo nimeongea na hawa viongozi, na nimeambia waziri wangu apange vile tutahakikisha kwamba zile security roads ndogo ndogo tumetoa milioni 100 kutengeneza barabara za maram ambazo zitakubaliana na viongozi wenu. Jambo la pili kuhusu hiyo mambo ya barabara vile vile, nimezungumza na marafiki wetu wengi wakiwemo watu wa World Bank na wengine, na tena tumepata pesa bilioni mbili ya barabara za Marsabit. Um, kuna barabara ya kutoka Loglogo kwenda mpaka Kargi. Hapo tumeweka milioni 380, na tayari contractor yuko pale. Nataka itengenezwe. Tulimobilize hii mwezi wa nne, nataka itengenezwe, na mimi nitakuja mwenyewe pale kuja kuziangalia. Eh, kuna barabara pia ya North Horr kwenda mpaka Dukana. Hiyo barabara vile vile tumeweka ni karibu kilomita 30, tumeweka milioni 350. Huyu mbunge wetu, Bwana Walio, anajua. Um, na pia tumemobilize contractor, tunafanya na watu wa EU na watu wa AFD tuweze kutengeneza hiyo barabara iweze kupitika. Vile vile, tumeweka pesa ingine karibu shilingi bilioni moja kwa barabara ya Sololo, Anona, Golole, Uran. Nyinyi mnajua hiyo barabara.
A
Audience41:21
Ya kutoka Sololo mpaka Uran.
W
William Ruto41:25
Na tayari, mimi nitakuja hapo kwa sababu contractor amepatikana, na tutajenga hiyo barabara. Mnanielewa? Na mimi nataka niwaulize hao wabunge wetu na gavana, na mnisaidie na senator, mnisaidie kufuatilia, si ndio? Na mimi nitakuwa hapo kuja kuziangalia hizo barabara ndio tuweze kusonga pamoja. Um, kuna barabara ingine inaitwa Manyata Jilo, sijui Manyata Jilo ni wapi hapa? Eh, Manyata Jilo, si ndio? Na mahali inaitwa Gorugesa. Mnajua, hiyo barabara vile vile nimeweka milioni 100, nataka tutengeneze hiyo barabara yenu. Na tayari kandarasi tumemaliza, na contractor amepatikana, tunakuja kutengeneza hizo barabara. Watu wa Marsabit, mnanielewa? Eh, vile vile nataka mnisikize kwa makini, kwa sababu mnajua mimi ni mfanyikazi wenu, si ndio? Na saa zingine msiponiona kule Marsabit, pengine mnashangaa kama mimi nimewasahau. Mimi siwezi kuwasahau. Hata kabla, hata kama sijafika, mambo yenu mimi napanga, na mpaka itafaulu, kwa sababu nyinyi ni watu wangwana, na nyinyi ni watu wazuri, na nyinyi ni watu ambao tunaaminiana pamoja. Kuna mambo mawili ya muhimu. Nilikuwa pale Loyangalani, na mkanieleza ya kwamba hii wind power, Turkana wind power, iko karibu na Loyangalani, lakini Loyangalani haina stima. Sasa nimeweka pesa ya serikali milioni 390, na kabla ya Desemba tutakuwa tunawasha mataa hapo Loyangalani. Tutakuwa tumeleta stima hapo kutoka hapo Loiyangalani. Najua viongozi hawa wameniuliza pia tusukume hiyo stima iende Marsabit na iende Sololo. Hiyo bado iko kwa napangia. Kuna safari lazima niende ndio nipange vizuri, nipate pesa ya kutosha ndio nifanye hiyo kazi. Lakini hata na hivyo, iko sawa. Vile vile hapo Loyangalani, tulikubaliana ya kwamba tuunganishe Loyangalani na Loiyangalani, na mambo ile tuweke ferry kama ile iko Mombasa kule. So um, nimekubaliana na watu wa Kenya Ports Authority, na tutakuja hapa ni ya kwamba hiyo ferry tayari tumetoa pesa ya kujenga hiyo ferry ya kuunganisha watu wa Turkana na watu wa Marsabit. Na tutajenga pale mahali pa hiyo ferry kutua. We need about 400 million, tayari we have it in the budget. Ng'ambo hii 400, ng'ambo ile 400 million, na 700 ya kutengeneza hiyo ferry, na hiyo itafanyika mwaka huu. Tunaelewana? Pia nyinyi mnajua tuko na biashara kubwa inaendelea kati ya Kenya na Ethiopia pale Moyale. Pale Moyale tunahitaji dry port, si ndio? Ya kusukuma biashara pale Moyale. Huyu gavana wenu ako na barua yangu, nimemwandikia. Tunataka shamba ekari 200. Mimi niko na pesa ya kutengeneza dry port. Na gavana na watu wa County Assembly, mumalize hiyo kazi, mkinitumia next week, basi mimi nitakuja pale na contractor wa kutengeneza dry port ndio tuendelee na biashara kati ya Kenya na Ethiopia. Tumekubaliana. Tuko na program ya affordable housing ambayo inaendelea. Mimi nataka niwahakikishie ya kwamba katika mipango yetu, tumeweka Marsabit County tumeweka shilingi bilioni saba ya affordable housing, ya masoko, na ya hostels. Kati ya sehemu ambazo tumezipangia, ni kwamba hapo Saku najua mnajua inaendelea saa hizi. We have already awarded a 700 million program ya affordable housing. My corner, tumeaward tayari eh, affordable housing ya shilingi bilioni moja pale Myona. Eh, tumekubaliana tunaweka affordable housing kama Samis, North Horr, Sololo vile vile tumewapangia mambo ya affordable housing. Masoko, tuko na fish market ambayo tayari tumepata contractor ya shilingi milioni 190 Loyangalani. Tumepanga soko ya Turbi, Laisamis, Karare, Uran, na Bubisa. Yote haya tunajenga. Masoko, watu yangu ya affordable housing wanapangia nyinyi hiyo kazi. Hostels ya vijana wetu, tumesema vijana wale wako kwa TVET, vijana wale wako kwa KMTC, na vijana wale wako katika program hizo, pia tuwajengee hostel. Katika mipango yetu, tunajenga hostels vijana 1,500 Marsabit. Na Saku TVET tayari eh, hostel inaendelea. Obo, North Horr, Laisamis, na Saku KMTC iko katika procurement, ndio tuhakikishe hawa vijana wetu wanaosoma pale pia wanapata nafasi ya kusoma. Pia eh, gavana hapa ameniuliza kwa niaba ya viongozi hawa wote wa Marsabit ya kwamba mnataka pia kaunti ya Marsabit ipate nafasi ya kuwa na university, si ndio? Lakini sasa, hii university tutaanzia wapi? Eh, mimi nataka niwapatie mpango ya kuwa na university, si ndio?
Ngoja, ngoja, ngoja, ngoja, ngoja. Unajua shida yenu ni mashindano kila wakati. Eh, so eh, nimeshaongea, nimeshaongea na university yetu ya Egerton University, kwa sababu wao ndio wanafanya mambo mengi ya ufugaji. Nyinyi mnanielewa? Nimeshaongea na wao, na tayari tumekubaliana. Wameenda wakafanya maneno maneno mahali inaitwa Karare hapo. Ah, nataka kwanza tutaanza hivi. Sikizeni, nataka mjue vile tutaanza. Tutaanza na kuwa na constituent campus. Na tayari nimeambia wizara, tutajenga hostels, na tutajenga administration block, na tutajenga tuition block. Tumeweka pesa ya kwanza shilingi milioni 500 ndio tuanze. Na mimi nitakuja hapo nikikuja Marsabit mwezi wa nane hivi, nitakuja kuianzisha ndio tuanze kuijenga. Nyinyi mnanielewa? So mpangane hapo, alafu sasa nitajua vile nitasongesha kutoka hapo. Pia hawa viongozi wameniuliza ya kwamba mnataka hospitali level 6. Hapo tayari wanajua, nilikuwa nchi ya Italy karibu miezi miwili iliyopita, na tumekubaliana na serikali ya Italy tutafanya kwa pamoja na serikali ya Kenya, na tayari tumeidentify hospitali ya shilingi 1.3 billion ya Marsabit. Huyu gavana wenu, gavana wenu anajua, si unajua Abshiro? Eh, anajua. Anajua ya kwamba hiyo mpango tuko nayo. Nimemueleza kuna mambo lazima kaunti wafanye. Wakifanya mambo yao, mimi nitafanya mambo yangu, alafu tutakuja. Eh, bado kuna stages mbili hapo katikati. Lazima tupeleke bunge. Kuna maneno lazima ifanyike hapo bunge kidogo. Nitaharakisha, wewe Raso na eh, mama Naomi, na Mheshimiwa wa Moyale, na Wario, mtapangana alafu tutasonga namna hiyo pamoja, alafu ndio tumalize hiyo maneno, ndio tuweze kuwa na hospitali kubwa ambayo itasaidia watu wa Marsabit. Tunajua tumejenga ile ya Sololo, tumefanya equipment, kaunti walijenga, tumeequip, na kazi zile zingine zinaendelea pale. Mambo ya maji tumekubaliana. Badasa damu ni kweli imechelewa, imechelewa muda mrefu. Tulikuwa na kesi, tukawa na matatizo, lakini haya makesi yote sasa tumeyatatua, na nimeambia wizara ya kwamba tutafute pesa ya kwanza ya kuanzisha, na nyinyi mtaona tu hivi karibuni hiyo kazi itaanza. Tumekubaliana ya kwamba Uri Hills pia tuweke damu kubwa pale. Eh, ilikuwa inaitwa Kalacha, Kalacha, Uri Hills, tuweke hapo damu. Tumesema tuweke damu ingine Sololo ya kusaidia kupanga sehemu hiyo. Na tumekubaliana pia Core, Loglogo, tuweke damu ingine. Nyinyi mnajua, kwa mambo ya maji, sikizeni, kwa mambo ya maji mimi nimesema ile National Infrastructure Fund yake kubwa ni kazi tatu: number one, transport and logistics; number two, energy generation; na number three, water storage, water harvesting and irrigation. Kwa hiyo water storage, water harvesting and irrigation iko mpango yetu kamili ya mambo ya maji ya Marsabit kwa hiyo National Infrastructure Fund. Kwa hivyo tutapangana na nyinyi hapo na tuhakikishe ya kwamba kazi hiyo inaendelea. Kwa mambo ya mining, watu wa Marsabit, Mungu amewabariki, mko na raslimali ya mining. Kumekuwa na matatizo kidogo pale, fujo, nini, watu wamekuja wakora wengine kutoka nchi zingine, nini nini, ikabidi tuzuie kidogo. Lakini nimeamrisha Joho na watu wa ministry ya mining kwamba in minus wapatiwe leseni zao waendelee na kufanya biashara yao. Alafu ile ingine tutapangana na wale wengine, na nyinyi pia mjipange mbali na artisanal miners, pia na nyinyi muunganishwe katika ile mining ya mambo makubwa makubwa, pia na nyinyi muwe huko ndani, na kaunti ya Marsabit iwe katikati ya hiyo mpango. Tumeelewana jameni? Ili royalties ikikuja itakuja kwenu, ile levies ikikuja inakuja kwenu, lakini hata naye biashara hiyo ingine ikuje pia kwa watu wa Marsabit, ndio tuweze kutembea kwa pamoja. Marsabit, tumekubaliana.
A
Audience56:29
Watu wa Marsabit, tumekubaliana.
W
William Ruto56:34
Mambo ya barabara nimewaeleza, kama kuna na ingine itabaki tutafanya na hawa viongozi wenu. Maneno ya maji tumekubaliana, ile ingine imebaki tutashirikiana na hawa viongozi wenu. Na hawa viongozi wenu hawahitaji appointment ya kuja kuniona, so hawa watu wanakuja hapa wakitaka, si ndio? Tumekubaliana vile vile maneno yenu ya matibabu, kila mtu ajiandikishe kwa SHA ndio niweze kupanga vizuri mambo yenu ya matibabu. Sitaki mtu auze shamba ama ng'ombe ama mifugo ati kulipa gharama ya hospitali. Gharama ya hospitali tunataka isimamiwe na serikali ya Kenya. Tumekubaliana na nyinyi pia msomeshe watoto wenu. Hatutaki mtoto wa kwenda shule aende achunge ng'ombe ama mbuzi. Hapana. Wakati wa shule, watoto wote waende shule. Tumekubaliana na nyinyi maneno ya stima. Tayari nataka mnisikize kwa mambo ya stima. Mbali na yale tumesema kuhusu eh, maneno ya grid, pia kwa bajeti yetu ya mwaka huu tuko na 2.81 billion shillings ya watu wa Marsabit kuwaunganisha stima. Ile ya last mile, tuko na mini grid. Na mjue umuhimu ya mini grid. Umeme na wind ndio itakuwa stima ya siku zijazo. Na tumekubaliana tunaweka mini grid. Tumewapatia pesa shilingi bilioni moja ya kujenga mini grids Marsabit County. Tunaweka mini grid mahali inaitwa Elbor, nyinyi mnajua mahali Elbor iko. Tunaweka mini grid Dildima, Bori, Forole, Kargi, Gas, kuna mahali inaitwa Gas. Gas gani hii tena? Gas. Alafu Elgedi, Bubisa, Gadab, na eh, South Horr tunaweka vile vile. Um, eh, tunaweka vile vile mini grid. Na hiyo mini grids yote tayari tumepatiana kandarasi, saa ingine inaendelea kujengwa. Mimi nimesema in the next two months nataka zile za kwanza ziwe zimekamilika. Nyinyi muhakikishe stima na mkae kama watu wengine wa taifa letu. Tunaelewana? Tumekubaliana tuweke mini grid Bubisa, si namna hiyo? Tuweke ingine, dunia hiyo ingine yote, si namna? Na kazi hilo zingine zote tutashirikiana. Kuna maneno ambayo hatujasema leo. Mimi nitakuja Marsabit niketi chini ya miti mnieleze. Si ndio? Najua mko na maneno. Si mimi najua mko na maneno. Leo ilikuwa siku yangu kwa sababu nyinyi ni wageni wangu. Sasa nitakuwa mgeni wenu. Sasa mjipange na maneno yenu mkuje mnieleze. Eh, mtakuja kunieleza. Nyumbani nikikuja.
A
Audience1:00:29
Ndio.
W
William Ruto1:00:30
Nikuje siku ngapi? Ati wiki mbili. Eh, nitakuja, nitakuja, nitakuja at least siku tatu nikae hapo niangalie vile maneno yanaendelea, alafu tuongee ndio mniambie yenu. Hii ingine wacha mimi nipange nikamilishe ndio tuende mbele pamoja. Si namna hiyo?
A
Audience1:00:57
Marsabit hoye.
W
William Ruto1:00:59
Hoye.
A
Audience1:01:00
Marsabit hoye.
W
William Ruto1:01:02
Hoye. Mnasema tuendelee na hii kazi?
A
Audience1:01:05
Ndio.
W
William Ruto1:01:07
Nipange hii ya barabara nimalize?
A
Audience1:01:09
Ndio.
W
William Ruto1:01:10
Ya maji?
A
Audience1:01:11
Ndio.
W
William Ruto1:01:12
Ya kusomesha watoto?
A
Audience1:01:13
Ndio.
W
William Ruto1:01:14
Ya university.
A
Audience1:01:15
Ndio.
W
William Ruto1:01:16
Ya stima. Nipange hiyo yote. Hebu nione wale wanasema nipange hiyo maneno yote, si ndio? Na sikizeni, watu wa Marsabit, watu wa Marsabit, nataka muelewe ya kwamba mambo yenu ya Marsabit vile viongozi wenu wamesema hapa. Pale nyuma kulikuwa na ubaguzi. Pale nyuma, mtu wa Marsabit kupata kitambulisho ilikuwa ni kizungu mkuti. Unaulizwa maswali kutoka hapa mpaka Johannesburg. Lete kitambulisho ya huyu, lete ya yule, lete ingine. Nimesema ya kwamba ile maswali inaulizwa mtoto wa Kisumu na Eldoret na Kiambu na malingine, hiyo maswali kama ni mbili ama tatu, hiyo maswali uulizwe pia mtoto wa Marsabit, wakuwe sawa kama watoto wengine. Maneno ya vetting ya kuumiza watu wengine na kubagua watu wengine, nimesema hiyo ubaguzi ikome katika taifa letu. Sisi wote ni raia wa taifa letu la Kenya. Si namna hiyo jameni? Na mimi nataka niwahakikishie watu wa Marsabit, hamtasahaulika tena, hamtawachwa nyuma tena, hamtabaguliwa tena. Tutatembea tukiwa pamoja. Watu hawa mnaona wananipigia makelele, mimi ni kwa sababu nimesema tuwe na usawa katika taifa letu la Kenya. Nawauliza watu wa Marsabit, kuna makosa ya usawa? Kuna makosa ya watu wakisemekana wawe sawa? Si maendeleo ifike kila mahali ya Kenya? Ama mnasema namna gani? Si ndio? Yes. So tutaendelea na usawa. Tutapanga Kenya iwe sawasawa, na kila Mkenya ajihisi ya kwamba tuko katika taifa la Kenya. Na mimi nataka niwahakikishie, mbele na nyuma, kulia na kushoto, juu na chini, mambo ya ubaguzi haitawezekana tena katika taifa letu. We are going to move together as one people, as one nation. Tunaelewana? Hawa watu wanatupigia makelele mingi. They have no new ideas. Hawana mpango mbadala. Hawana maono, hawana sera, hawana agenda, hawana chochote. Wale mmeasikia mambo yao tu ni kuhangaika hapa na matusi, ati ile kazi kubwa wamefanya ni kunitafutia jina ati Kasongo. Wale watu wako chini sana bana. Mafala sana yaani. Sasa, you know, wacha niwaulize watu wa Marsabit, yaani ati ile kitu wanasema ati ya maana sana, ati nikandika mimi majina, sijui matusi, ukabila wanatuendeleka na chuki, wanatuletea ya ukabila. Mimi nimewaambia ya kwamba kama mnataka tushindane, tafuteni sera, tafuteni mpango, ama namna gani. Lakini hawana, they have no capacity. Yaani hawana capacity ya kudevelop. Capacity yao ni kupinga tu na matusi na ukabila na chuki na kuitana majina. Lakini hawa tutawanyorosha asubuhi sana. Hata hawajui Bubisa ni dunia gani, hawajui Korr iko wapi, hawajui Hills ziko wapi. They know nothing. Hawa ni watu bure. Sijui kama tunaelewana. Eh, mmewaona wale? Kwanza mwingine hata nilimuuliza, wewe sasa umekuwa kiongozi, umekuwa waziri wa everything wa hii Kenya, umekuwa waziri wa elimu, viwanda, sijui nini, foreign affairs, nini nini, na hiyo wizara yote ametangatanga huko, hakuna chochote inakumbukwa ati alifanya nini. Tu. Alafu sasa 50 years later, unasema ati umekuwa mwerevu all of a sudden. How? Sijui kama tunaelewana, my friends wa Marsabit. Tuendelee ama tuendelee?
A
Audience1:06:23
Si tuendelee.
W
William Ruto1:06:28
Wale jamaa niwaeleze, yaani maono ya Kenya hawana, agenda ya kupeleka Kenya yetu mbele hawana, sera ya kila kitu hawana, hata akili ya kupanga anything pia hiyo hawana. Sasa ni watu bure. Anyway, so um, wacha niseme kuzidi hapo. Mimi najua mmetembea safari ndefu, si ndio? Kwa sababu ya urafiki na kwa sababu ya mapenzi.